Kocha Mkongo wa Yanga asaini mkataba




Tangu ametua nchini, Zahera amekuwa akifanya kazi bila kuwa na mkataba, lakini leo Ijumaa jioni Mkongo huyo ametia wino mkataba wa miezi sita kuwanoa mabingwa hao wa msimu uliopita wa Ligi Kuu Bara. 
Lakini, Mwanaspoti ambalo limeshuhudia Mkongo huyo akimwaga wino, linafahamu kuwa kuchelewa kusaini mkataba huo ni sehemu ya makubaliano yake na mabosi wa Yanga.
Pia, Mwanaspoti linafahamu kuwa mara baada ya kusaini mkataba huo, Zahera alikwea pipa kwenda kwao DR Congo na atarejea ndani ya siku chache zijazo kuendelea na majukumu yake.


Share on Google Plus

About Chagaboy

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

1 comments:

  1. Mchana mwema, wewe vipi? Mimi ni Mbrazil na ninatafuta wafuasi wapya wa blogi yangu. Naweza kukufuata pia. Marafiki wapya pia wanakaribishwa.

    https://viagenspelobrasilerio.blogspot.com/?m=1

    ReplyDelete